Headlines News :
Home » » MANCHESTER UNITED YATANDIKWA 2-1 NA REAL MADRID KWENYE MCHEZO WA KIRAFIKI

MANCHESTER UNITED YATANDIKWA 2-1 NA REAL MADRID KWENYE MCHEZO WA KIRAFIKI

Written By kunta kinte on Monday, June 3, 2013 | 3:03 PM


Mechi ya Kirafiki Maalum iliyoshirikisha Manguli wa Klabu za Manchester United na Real Madrid ili kusaidia Mfuko wa Hisani wa Klabu ya Manchester United uitwao RED HEART UNITED na Real waliibuka kidedea kwa kushinda Bao 2-1.

Kabla ya Mechi hiyo kuanza, kulikuwa na utangulizi wa Shoo Laivu ya Muziki iliyofanywa na Mastaa JLS na Amelia Lily.

Real ndio walitangulia kupata Bao lililofungwa na Morientes katika Dakika ya 40 kwa shuti la nje ya Boksi lililomshinda Kipa Edwin Van Der Sar.
Man United walisawazisha katika Dakika ya 67 baada ya Andy Cole kumtengenezea Ruud Van Nistelrooy aliefunga kwa Shuti kali.

Van Nistelrooy alianza Mechi hii kwa kuichezea Real Kipindi cha Kwanza na Kipindi cha Pili kuvaa Jezi ya Man United.

Bao la ushindi kwa Real lilifungwa na Ruben De Le Red katika Dakika ya 84 alipomhadaa Kipa Van Der Gouw alieingia kuchukua nafasi ya Edwin Van Der Sar


Mchezaji wa siku nyingi wa Man United Jaap Stam akichuana na mchezaji wa Real Madrid

Zinedine Zidane akitaka kumtoka Denis Irwin

Ruud van Nistelrooy akipongezwa na wachezaji wa United baada ya kuwapatia bao

Real Madrid wakimpongeza mchezaji wa zamani wa Liverpool Fernando Morientes

Dwight Yorke akiachia shuti kali mbele ya Francisco Pavon

Claude Makelele kwenye patashika na Paul Scholes akiwa chini hapa, hakika ilikuwa ni fulu burudani

Mechi ilikutanisha wakongwe wazamani katika vilabu vyote kati ya Real Madrid na United

Kipa wa Zamani wa United Edwin van der Sar akishangaa baada ya kufungwa bao

Andy Cole na yeye alikuwa mstari wa mbele kwenye mechi ya Maveteran leo hii.
VIKOSI:
Manchester United: Van der Sar, van der Gouw; Berg, Blackmore, Irwin, Johnsen, Martin, Stam; Fortune, Robson, Scholes, Sharpe; Cole, van Nistelrooy, Yorke.

Real Madrid:
Contreras, Sanchez; Cannavaro, Helguera, Hierro, Pavon, Salgado, Sanz; Amavisca, De la Red, Figo, McManaman, Makelele, Zidane; Alfonso, Butragueno, Morientes, van Nistelrooy.
Share this article :

0 comments:

Speak up your mind

Tell us what you're thinking... !

Popular Posts

Comments

blogs zinazotamba

Translate

Popular Post

Flag Counter
 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Proudly powered by Blogger
Copyright © 2011. NDOANO YA HABARI - All Rights Reserved
Template Design by Creating Website Published by Mas Template