Korea Kaskazini leo imefyatua makombora matatu ya masafa mafupi ndani
ya Bahari ya Japan, kama sehemu ya mazoezi ya kijeshi. Msemaji wa wizara
ya ulinzi ya Korea Kusini amesema makombora mawili yalifyatuliwa mapema
leo na jingine moja likafyatuliwa saa za mchana. Amesema Korea Kusini
inaendelea kuwa katika hali ya tahadhari ili kupambana na hali yoyote ya
kitisho inayoweza kusababishwa na serikali ya Korea Kaskazini. Majaribio
hayo yanafuatia mazoezi ya pamoja yaliyofanywa na jeshi la wanamaji la
Marekani na Korea Kusini mapema wiki hii, na kushutumiwa na Korea
Kaskazini kuwa ni uchokozi na matayarisho ya vita.
Home »
habari ya kimataifa
» KOREA KASKAZINI YAONYESHA KIBULI KWA WAPINZANI WAKE KWA KUFYATUA MAKOMBOLAYAKE KATILKA NCHI YA JAPAN
KOREA KASKAZINI YAONYESHA KIBULI KWA WAPINZANI WAKE KWA KUFYATUA MAKOMBOLAYAKE KATILKA NCHI YA JAPAN
Written By kunta kinte on Saturday, May 18, 2013 | 3:05 PM
Labels:
habari ya kimataifa
0 comments:
Speak up your mind
Tell us what you're thinking... !