Headlines News :
Home » » URUSI YAJIPANGA KULUDISHA AMANI SYRIA

URUSI YAJIPANGA KULUDISHA AMANI SYRIA

Written By kunta kinte on Friday, May 10, 2013 | 2:46 PM


Rais  wa  Urusi Vladimir  Putin  amesema  leo  kuwa  amejadiliana na  waziri  mkuu  wa  Uingereza David Cameron  uwezekano na hatua  za  pamoja  za  kumaliza  mzozo  nchini  Syria. cameron aliwasili  leo  katika  mji  wa  Sochi, kusini  mwa  Urusi kwa majadiliano  na  rais Putin kuhusiana  na  hatua  za  kuchukuliwa kumaliza  mzozo wa  vita  vya  wenyewe  kwa  wenyewe  nchini Syria.
Wakati huo huo Kamishna  wa  haki  za  binadamu  wa  Umoja  wa mataifa  Navy Pillay  ameeleza  wasi  wasi  wake  kuhusu kupelekwa  kwa  majeshi  ya  Syria  karibu  na  mji   unaoshikiliwa  na waasi  wa  Qusair  magharibi  ya  nchi  hiyo. Mji huo umezingirwa na majeshi ya Syria kwa wiki kadhaa sasa na waasi wamepoteza nguvu za kulidhibiti eneo hilo.
Pillay alisema mauaji ya halaiki ya wiki iliopita yanapaswa kutoa chachu kwa jumuiaya ya kimataifa itafute suluhisho la haraka la mzozo huo wa miezi 26 sasa nchini Syria.
Share this article :

0 comments:

Speak up your mind

Tell us what you're thinking... !

Popular Posts

Comments

blogs zinazotamba

Translate

Popular Post

Flag Counter
 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Proudly powered by Blogger
Copyright © 2011. NDOANO YA HABARI - All Rights Reserved
Template Design by Creating Website Published by Mas Template