Polisi nchini Tanzania imesema leo kuwa imewakamata watu watano waliopatikana na mabomu katika mji mkuu wa kibiashara wa Dar es Salaam. Mkuu wa Jeshi la Polisi Suleiman Kova amesema watu hao watano walikamatwa siku ya Alhamisi baada ya polisi kudokezwa na wananchi. Kova amesema uchunguzi unaendelea kubainisha ni kwa nini watu hao walikuwa na mabomu na walikusudia kuyapeleka wapi. Mnamo Mei 5, palitokea shambulizi la bomu katika kanisa moja la Katoliki mjini Arusha ambapo watu watatu waliuawa na wengine 60 wakajeruhiwa. Gazeti la kila siku la Habari Leo, ambalo lina uhusiano wa karibu na serikali, limesema washukiwa hao watano waliokamatwa ni raia wa Tanzania.
Home »
habari ya kitaifa
» RAIYA WAKAMATWA NA MABOMU TANZANIA
RAIYA WAKAMATWA NA MABOMU TANZANIA
Written By kunta kinte on Saturday, May 18, 2013 | 3:23 PM
Polisi nchini Tanzania imesema leo kuwa imewakamata watu watano waliopatikana na mabomu katika mji mkuu wa kibiashara wa Dar es Salaam. Mkuu wa Jeshi la Polisi Suleiman Kova amesema watu hao watano walikamatwa siku ya Alhamisi baada ya polisi kudokezwa na wananchi. Kova amesema uchunguzi unaendelea kubainisha ni kwa nini watu hao walikuwa na mabomu na walikusudia kuyapeleka wapi. Mnamo Mei 5, palitokea shambulizi la bomu katika kanisa moja la Katoliki mjini Arusha ambapo watu watatu waliuawa na wengine 60 wakajeruhiwa. Gazeti la kila siku la Habari Leo, ambalo lina uhusiano wa karibu na serikali, limesema washukiwa hao watano waliokamatwa ni raia wa Tanzania.
Labels:
habari ya kitaifa
0 comments:
Speak up your mind
Tell us what you're thinking... !